728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, October 05, 2014

    FLAMINI AJUTA KUTOTWAA MATAJI AKIWA NA FABREGAS ARSENAL



    Kiungo Mathieu Flamini bado anaendelea kujuta kuhusu Fabregas.Hajuti kwa kuwa Fabregas hakurudi Arsenal kama alivyofanya yeye ama kumuona akiwa kavaa jezi za blue za klabu ya Chelsea bali anajuta kutowahi kutwaa ubingwa wowote ule akiwa na rafiki yake huyo kipenzi.



     
    Wote walikulia Arsenal.Wakawa na kubaki marafiki wakubwa mpaka leo hii.Ni majirani katika jiji la London nyumba zao ziko pua na mdomo.


    Lakini Flamini anaikumbuka ile miaka ya furaha wakiwa pamoja Arsenal ambayo iliishia bila ya kumbukumbu yoyote ile ya ubingwa.

    Flamini anasema
    “Nilikuja hapa nikiwa na miaka 20,Fabregas alikuwa mdogo kwangu kwa miaka mitatu (3) imekuwa ni miaka kumi (10) sasa tangu kipindi hicho.
    Katika kipindi hicho tulipitia mambo mengi pamoja.Tulikuwa kwenye fainali ya ligi ya mabingwa mwaka 2006.Nimekuwa nikimpigania kwa miaka mingi.
    2007 wachezaji wa Arsenal wakiwa nyumbani kwa Malkia Elizabeth


    Wakati tuko pamoja hapa tulitengeneza uelewano mkubwa sana uwanjani.Alikuwa akishambulia sana huku mimi nikizuia sana,nikipambana kwa ajili yake.Jumapili nakutana nae haitakuwa rahisi kumkaba kwanza ni kwa sababu ni mchezaji mzuri na pia ni rafiki yangu kipenzi.

    Natamani tungewafunga Barcelona siku ile na kutwaa ubingwa wa Ulaya nikiwa sambamba nae ama ubingwa uliopita wa FA.Ni jambo gumu kumuona akiwa katika jezi za blue za Chelsea,ulikuwa ni uamuzi wake kwenda huko.Ni rafiki yangu bila kujali uamuzi aliouchukua bado nitaendelea kumuunga mkono.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: FLAMINI AJUTA KUTOTWAA MATAJI AKIWA NA FABREGAS ARSENAL Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top