728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, October 08, 2014

    PIGO ARSENAL OZIL NJE MIEZI MITATU



    Huenda mtu mwenye wakati mgumu kwa sasa katika duru za soka duniani akawa ni kocha wa klabu ya Arsenal Mfaransa Arsene Wenger akiwa bado hajapona maumivu ya kichapo cha bao mbili kwa nunge toka kwa klabu ya Chelsea, ndani ya muda mfupi uliopita amepoteza kiungo wake Mesut Ozil kutokana na majeraha ya goti.

     
    Chama cha soka cha Ujerumani kimesema kiungo huyo wa zamani wa Real Madrid alikosa kufanya mazoezi leo katika kambi iliyoko Frankfurt na kuelekea Munich akiwa na daktari wa timu hiyo Hans-Wilhelm Muller-Wolhlfahrt kufanyiwa
    vipimo vya MRI vilivyobaini tatizo hilo ambalo kupona kwake huchukua wiki 10-12.


    Kufuatia majeruhi hayo Ozil atakosa michezo miwili ya kusaka  tiketi ya kushiriki michuano ijayo ya Ulaya Euro 2016 dhidi ya Poland na Ireland huku akitarajiwa kuvaa tena jezi za Arsenal mwakani.Mbali ya Ozil majeruhi wengine wanaendelea kumuadhibu Arsene Wenger ni Olivier Giroud,Mathieu Debuchy,Theo Walcott,Aaron Ramsey,Abou Diaby na Yaya Sanogo.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: PIGO ARSENAL OZIL NJE MIEZI MITATU Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top