728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, December 02, 2014

    ZABALETA:LAMPARD KAMA KINDA LA MIAKA 18

    Mlinzi wa kulia wa klabu ya Manchester City Pablo Zabaleta ameibuka na kumwagia sifa kemkem nyota wa klabu hiyo Frank Lampard kufuatia kuisaidia klabu hiyo kuibuka na ushindi mnono wa goli 3-0 dhidi ya klabu ya Southampton katika dimba la St.Mary's juzi jumapili.

    Lampard aliingia kuchukua nafasi ya winga Jesus Navas na kufanikiwa kufunga goli la tatu baada ya kupokea pasi nzuri toka kwa mshambuliaji Sergio Kun Aguero na kufikisha jumla ya magoli 174 katika ligi ya Epl.

    Zabaleta akimzungumzia Lampard amesema 

    ``Lampard ni mchezaji wa mfano kwani licha ya kushinda mataji karibu yote akiwa na Chelsea bado ni mtu asiyeacha kupambana"
    ``Ni mchezaji wa kwanza kuja mazoezini na wa mwisho kuondoka,anafanya mazoezi kwa nguvu sana kama kinda wa miaka 18."
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ZABALETA:LAMPARD KAMA KINDA LA MIAKA 18 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top