728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, December 22, 2014

    WAAMUZI 11 BONGO WAULA FIFA

    Shirikisho la soka ulimwenguni FIFA limetoa
    orodha mpya ya waamuzi
    linaowatambua ,Kwenye orodha hiyo kuna
    jumla ya waamuzi 18 kutoka
    Tanzania,miongoni mwa waamuzi hao waamuzi
    11 wapya na 7 wa zamani.

    Waamuzi wapya wa kati kutoka Tanzania ni
    Mfaume Ali Nassor kutoka visiwani Zanzibar
    pamoja na Martin Saanya kutoka Morogoro,
    pia wamo waamuzi watatu wa kike ambao ni
    Florentina Zabron ,Jonesia Rukyaa pamoja na
    Sofia Ismail.

    Kwa upande wa waamuzi wasaidizi wanaume
    ni Frank John Komba na Soud Idd Lila , kwa
    upande wa wanawake ni Kudura Omary
    Maurice,Hellen Joseph Mduma,Dalila Jafari
    Mtwana na Grace Mawala.

    Waamuzi wa zamani wa Tanzania kwenye
    orodha ya FIFA ,kwa upande wa wanaume ni
    Israel Mujuni Nkongo na Waziri Sheha
    Waziri,kwa upande wa waamuzi wasaidizi ni
    Josephat Bulali,Fernand Chacha,John
    Longino Kanyenye ,Ali Kinduli na Samuel
    Hudson Mpenzu .

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WAAMUZI 11 BONGO WAULA FIFA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top