728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, December 30, 2014

    WAJUE MAKIPA WANAOLIPWA VIZURI ULAYA

    Wafuatao ni makipa wanaolipwa vizuri ulimwenguni.

    1-Iker Casillas
    Kipa Iker Cassilas wa Real Madrid ndiye
    anayeshika nafasi ya kwanza kwa
    kulipwa mshahara mkubwa duniani
    kwani kwa mwaka analipwa Pauni 6.3
    milioni.

    2-Manuel Neuer
    Kipa wa Bayern Munich, Manuel Neuer
    ndiye anayeshika nafasi ya pili kwa
    makipa wanaolipwa zaidi kwa sababu
    analipwa Pauni 5.6 milioni.

    3-Petr Cech
    Cech ni kati ya makipa bora katika Ligi
    Kuu ya England. Petr Cech analipwa na
    Chelsea mshahara wa Pauni 5.2 milioni
    kwa mwaka.

    4-Joe Hart
    Kipa wa Manchester City, Joe Hart
    ambaye amekuwa na misimu mizuri
    analipwa mshahara wa Pauni 4.68
    milioni kwa mwaka.

    5-Pepe Reina
    Kipa Pepe Reina wa Bayern Munich
    anashika nafasi ya tano kwa makipa
    wanaolipwa zaidi. Kiasi anacholipwa hivi
    sasa na Bayern ni Pauni 4.16 milioni kwa
    mwaka.

    6-David De Gea
    Kipa wa Manchester United, David De Gea
    hivi sasa yupo katika kiwango cha juu
    hivi sasa, klabu yake inamlipa mshahara
    wa Pauni 3.64 milioni kwa mwaka.

    7-Hugo lloris
    Kipa wa Tottenham, Hugo Lloris hivi sasa
    analipwa na klabu hiyo mshahara wa
    Pauni 3.59 milioni kwa mwaka.

    8- Gianluigi Buffon
    Kipa mzoefu wa Juventus, Gianluigi ‘Gigi’
    Buffon anashika nafasi ya nane katika
    makipa wanaolipwa mishahara mikubwa.
    Buffon analipwa mshahara wa Pauni 3.17
    milioni kwa mwaka.

    9-Claudio Bravo
    Kipa huyu wa klabu ya Barcelona
    analipwa na klabu hiyo Pauni 2.77
    milioni kwa mwaka.

    10-Salvatore Sirigu
    Kipa anayefunga orodha ya makipa
    wanaolipwa fedha nyingi ni kipa wa Paris
    Saint Germain, Salvatore Sirigu. Kipa
    huyu analipwa mshahara wa Pauni 2.6
    milioni kwa mwaka.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WAJUE MAKIPA WANAOLIPWA VIZURI ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top