728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, December 21, 2014

    KLOPP KAMA WENGER AENDELEA KUNG'ANG'ANIA DORTMUND LICHA YA VIPIGO

    Kocha mkuu wa klabu ya Borussia Dortmund Jurgen Klopp ameendelea kusisitiza kuwa hang'oki Dortmund licha ya klabu hiyo kuendelea kupokea vichapo kila uchao.

    Klopp ambaye aliiongoza Dortmund jana kupokea kichapo cha 10 cha msimu cha bao 2-1 toka kwa klabu nyingine inayosuasua ya Werder Bremer amesisitiza bado ataendelea kupigania kibarua chake licha ya kufanikiwa kuvuna pointi 15 katika michezo 17 ya ligi ya Bundesliga.

    Kichapo cha jana kimeiacha Dortmund katika nafasi ya pili mkiani huku ushindi wowote wa klabu ya Freiburg leo utaidondosha Dortmund mpaka mkiani kabisa mwa ligi hiyo ngumu duniani ambayo itasimama kwa wiki tatu kupisha sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KLOPP KAMA WENGER AENDELEA KUNG'ANG'ANIA DORTMUND LICHA YA VIPIGO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top