728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, December 21, 2014

    MAN CITY NOMA!!YAMTENGEA STERLING £60M ATUE ETIHAD

    Wakati klabu ya Liverpool ikihangaika kumshawishi nyota wake Raheem Sterling kumsaini mkataba mpya klabu ya Manchester City imeibuka na mpya baada ya kusema inapinga kubisha hodi klabuni hapo na ada ya £60m ili kumsajili nyota huyo wa pembeni.

    Sterling amebakiza miaka miwili ili kumaliza mkataba na majogoo hao wa jiji la Liverpool huku kukiwa na sintofahamu hasa juu ya lini nyota huyo atakubali mkataba mpya na hatimaye kubaki klabuni hapo.

    Mbali ya Manchester City vilabu vya Real Madrid na Bayern Munich navyo vimeonyesha nia ya kumnasa kinda  huyo mahiri mzaliwa wa Jamaica.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MAN CITY NOMA!!YAMTENGEA STERLING £60M ATUE ETIHAD Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top