728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, November 13, 2014

    TEGETE AIOMBA YANGA RUKSA ACHEZE NDONDO

    INAONEKANA kama uvumilivu
    umemshinda, kwani straika wa Yanga,
    Jerry Tegete ameomba viongozi wa timu
    za Ligi Kuu Bara kuwaruhusu wachezaji
    wao kucheza mechi za uswahilini
    maarufu kama ndondo ili kulinda vipaji
    vyao.

    Kauli hiyo ya Tegete imekuja baada ya
    klabu nyingi za Ligi Kuu kuwapiga
    marufuku wachezaji wao kucheza ndondo
    kwa hofu ya kuumia na kupata mzigo wa
    kuwatibu wanaporejea katika timu.

    Tegete alisema kwa mfano hivi sasa ligi
    imesimama na wachezaji wako
    mapumzikoni ambako hawawezi
    kujibweteka, wanafanya mazoezi katika
    timu za mitaani lakini wanapata wakati
    mgumu kucheza mechi kwani
    hawaruhusiwi na waajiri wao.
    Straika huyo anafanya mazoezi binafsi
    kutetea nafasi yake Yanga ambayo mmoja
    kati ya wachezaji wanaomuweka benchi
    ni Genilson Santos ‘Jaja’ wa Brazil.
    “Mimi naomba turuhusiwe kucheza mechi
    za uswahilini ili kukuza viwango kwani
    bila hivyo tutapoteza vipaji vyetu kwani
    muda wa wiki nne kukaa bila kucheza si
    vizuri.

    “Sisi ni binadamu na huku tunapoishi
    kuna timu tunazofanya nazo mazoezi sasa
    kama umeshiriki mazoezi halafu siku ya
    mechi hauendi kucheza hapo hautengenezi
    picha nzuri kwa jamii hasa katika
    uhusiano, tulipaswa kusisitizwa kucheza
    kwa uangalifu tu,” alisema Tegete.

    Mara nyingi Tegete huwa anafanya
    mazoezi na baadhi ya wachezaji wa Ligi
    Kuu na Daraja la Kwanza katika timu ya
    Tabata FC kama David Luhende wa
    Mtibwa Sugar, Godfrey Taita (Mwadui FC)
    na Ivo Mapunda wa Simba.

    Kwa mujibu wa habari za ndani, mchezaji
    yeyote wa Yanga akithibitika kucheza
    ndondo anakatwa Sh400,000 katika
    mshahara wake.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TEGETE AIOMBA YANGA RUKSA ACHEZE NDONDO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top