728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, November 13, 2014

    BABA:KIEMBA ONDOKA SIMBA

    SHABAN Ramadhan Kiemba ‘Shundu’
    ambaye ni baba mdogo wa kiungo wa
    Simba, Amri Kiemba, ameiomba klabu
    hiyo kuachana na mwanaye kuliko kukaa
    na kumpakazia maneno ya uongo
    yanayomchafua katika jamii.
    Kiemba pamoja na wachezaji wengine
    wawili; Shaban Kisiga na Haroun
    Chanongo, wamesimamishwa na uongozi
    wa klabu hiyo kwa madai ya kucheza
    chini ya kiwango na kuihujumu timu.

    Shundu alisema: “Mwanangu (Amri
    Kiemba) anateseka sana na hizo tuhuma,
    si kweli kwamba anacheza chini ya
    kiwango akiwa Simba, ni mfumo ndiyo
    tatizo, madai wanayotoa viongozi si ya
    kweli kabisa.

    Akiwa Taifa Stars anacheza katikati, kazi
    yake inakuwa kupeleka mashambulizi na
    kusaidia kukaba kwa wakati fulani, akiwa
    Simba wanamtumia pembeni, ni nafasi
    mbili tofauti na huwezi kutegemea ufanisi
    unaofanana.”
    Kitaaluma Shundu ni kocha na amewahi
    kuzifundisha timu kadhaa nchini kama
    zikiwamo AFC na Palsons za Arusha,
    Lipuli ya Iringa na Kahama United ya
    Shinyanga.

    “Ni bora wakamwacha tu, hajaniambia
    kuwa anataka kwenda wapi lakini ni bora
    akaenda Azam ama Yanga,” aliongeza.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: BABA:KIEMBA ONDOKA SIMBA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top