728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, November 14, 2014

    NDUGU WA GERVINHO ATUA AZAM FC

    Dar es Salaam. Wakati beki wa kimataifa
    kutoka Ivory Coast, Paschal Serge Wawa
    akimwaga wino mkataba wa miaka
    miwili kuichezea Azam, Simba imekataa
    maombi ya Azam kumsajili kiungo Amri
    Kiemba kwa mkopo.

    Wakala wa mchezaji huyo aliwasili jana
    akitokea Ivory Coat tayari kwa
    mazungumzo ya mwisho na kusaini
    mkataba na mmiliki wa timu hiyo,
    Kampuni ya Said Salim Bakhressa.
    Wawa ambaye tayari alishafanyiwa
    vipimo vya awali vya uchunguzi wa afya
    yake alikuwa akiichezea El Merreikh ya
    Sudan, amechukua nafasi ya Ismailla
    Diara kutoka Mali anayefungashiwa
    virago na klabu hiyo kutokana na
    kuonyesha uwezo mdogo.

    Azam, tayari imeiandikia barua Simba
    ikimtaka Kiemba ambaye amesimamishwa
    na klabu hiyo kwa madai ya utovu wa
    nidhamu.
    Kwa upande wo, Azam wanamtaka
    Kiemba kwa mkopo, kitu ambacho Simba
    wamekigomea na kutaka wamnunue moja
    kwa moja, wala si kumchukua kwa
    mkopo.

    Hadi sasa, Kiemba ana mkataba wa
    mwaka mmoja wa kuitumikia klabu hiyo
    ya Wekundu wa Msimbazi. Mmoja wa
    viongozi wa Azam aliwarushia kijembe
    Simba akisema:

    “Simba ni watu wa ajabu, lengo lao ni
    kumkomoa mchezaji kwani ni wazi
    hawamtaki, lakini wanamng’ang’ania,
    wakati hawatamtumii, sisi tupo tayari
    kumchukua kwa mkopo.”
    Awali, Kiemba alikuwa akiwaniwa na
    Yanga msimu uliopita, lakini Simba
    walipogundua hilo waliwahi na
    kumsanisha mkataba wa miaka miwili.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: NDUGU WA GERVINHO ATUA AZAM FC Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top