728x90 AdSpace

  • Latest News

      Friday, November 14, 2014

      NDUGU WA GERVINHO ATUA AZAM FC

      Dar es Salaam. Wakati beki wa kimataifa
      kutoka Ivory Coast, Paschal Serge Wawa
      akimwaga wino mkataba wa miaka
      miwili kuichezea Azam, Simba imekataa
      maombi ya Azam kumsajili kiungo Amri
      Kiemba kwa mkopo.

      Wakala wa mchezaji huyo aliwasili jana
      akitokea Ivory Coat tayari kwa
      mazungumzo ya mwisho na kusaini
      mkataba na mmiliki wa timu hiyo,
      Kampuni ya Said Salim Bakhressa.
      Wawa ambaye tayari alishafanyiwa
      vipimo vya awali vya uchunguzi wa afya
      yake alikuwa akiichezea El Merreikh ya
      Sudan, amechukua nafasi ya Ismailla
      Diara kutoka Mali anayefungashiwa
      virago na klabu hiyo kutokana na
      kuonyesha uwezo mdogo.

      Azam, tayari imeiandikia barua Simba
      ikimtaka Kiemba ambaye amesimamishwa
      na klabu hiyo kwa madai ya utovu wa
      nidhamu.
      Kwa upande wo, Azam wanamtaka
      Kiemba kwa mkopo, kitu ambacho Simba
      wamekigomea na kutaka wamnunue moja
      kwa moja, wala si kumchukua kwa
      mkopo.

      Hadi sasa, Kiemba ana mkataba wa
      mwaka mmoja wa kuitumikia klabu hiyo
      ya Wekundu wa Msimbazi. Mmoja wa
      viongozi wa Azam aliwarushia kijembe
      Simba akisema:

      “Simba ni watu wa ajabu, lengo lao ni
      kumkomoa mchezaji kwani ni wazi
      hawamtaki, lakini wanamng’ang’ania,
      wakati hawatamtumii, sisi tupo tayari
      kumchukua kwa mkopo.”
      Awali, Kiemba alikuwa akiwaniwa na
      Yanga msimu uliopita, lakini Simba
      walipogundua hilo waliwahi na
      kumsanisha mkataba wa miaka miwili.

      • Blogger Comments
      • Facebook Comments

      0 comments:

      Post a Comment

      Item Reviewed: NDUGU WA GERVINHO ATUA AZAM FC Rating: 5 Reviewed By: Unknown