728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, November 06, 2014

    KOMBE LA DUNIA 2022 SHAKANI

    Rais wa shirikisho la vyama vya soka barani
    Ulaya-Uefa, Michel Platini amesema kuwa
    fainali za kombe la dunia za mwaka 2022
    nchini Qatar lazima zichezwe kipindi cha
    majira ya baridi.

    Mchezaji huyo wa zamani wa Ufaransa
    amejiweka katika upinzani dhidi ya baadhi ya
    vilabu vikubwa vya soka barani Ulaya
    ambavyo vimesisitiza kuwa fainali hizo
    zipangwe mwezi May 2022.
    Kwa kawaida fainali za Fifa za kombe la
    dunia huwa zinachezwa kati ya mwezi Juni na
    Julai, lakini Fifa imeambiwa kuwa katika
    majira hayo nchini Qatar kunakuwa na joto
    kali litakalowaweka wachezaji kwenye hatari
    kiafya.

    Platini ameiambia BBC kuwa “haiwezi kuwa
    mwezi Aprili, Mei wala Juni, bali itakuwa
    wakati wa majira ya baridi tu,” na kuongeza
    kuwa mwaka 2022 michezo ya nusu fainali na
    fainali ya Ligi ya mabingwa Ulaya inaweza
    kusogezwa hadi mwezi Juni ikiwa ni lazima,
    na kwamba vilabu vinapaswa kukubali uamuzi
    wowote utakaokuwa umekubaliwa.

    “Sio vilabu ambavyo vinacheza, ni wachezaji
    na sio rahisi kucheza mwezi Mei ambapo
    kuna joto la hadi 40c” Alisema Platini
    mwenye umri wa miaka 59.
    Mivutano
    Itakumbukwa kuwa Qatar ndiyo ilishinda haki
    ya kuwa mwenyeji wa fainali hizo za mwaka
    2022 na tangu imeshinda kumekuwa na
    mivutano miongoni mwa wadau mbalimbali
    kuhusu uwezekano wa kuchezwa nchini humo
    kutokana na hali ya hewa ya joto kali.

    Sepp Blatter
    Rais wa Fifa Sepp Baltter amekuwa
    akituhumiwa na baadhi ya watu kuwa
    ameipendelea Qatar katika mchakato huo.
    Vilabu vikubwa vya ligi kuu ya England, La
    Liga ya Hispania na Bundesliga ya Ujerumani
    vinadhani kuwa mwezi Mei kutakuwa na nafuu
    kiasi wakati ambapo Fifa yenyewe inashikilia
    msimamo wa kutafuta uwezekano wa miezi ya
    Juni na Julai kama kawaida.

    Wadau mbalimbali wenye ushawishi mkubwa
    katika soka duniani walikutana jumatatu mjini
    Zurich katika harakati za kujaribu kupata
    suluhu ya mgogoro huu mkubwa wa aina yake
    ulioiweka Fifa njia panda, na wamepanga
    kukutana tena mwezi Januari 2015.

    Kikosi kazi kimeundwa ili kutafiti na kutoa
    mapendekezo yake kwa kamati ya utendaji ya
    Fifa mwezi Machi mwaka ujao, huku
    pendekezo la Fifa likiwa ni kusogeza fainali
    hizo hadi mwezi Novemba na Desemba 2022.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KOMBE LA DUNIA 2022 SHAKANI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top