728x90 AdSpace

  • Latest News

      Saturday, November 01, 2014

      TFF YATAKA JEZI MPYA STARS

      Shirikisho la soka Tanzania, TFF, limesema
      linakaribisha wabunifu watakaobuni
      mwonekano wa jezi mpya za timu ya taifa kwa
      mechi za nyumbani na ugenini.
      Hata hivyo sharti la ubunifu huo lazima
      uzingatie rangi za bendera ya taifa ambazo ni
      kijani, njano, nyeusi na bluu.

      Wakati tangazo hili likitolewa na TFF, tayari
      uongozi mpya chini ya rais wake Jamal
      Malinzi umebadili jezi zinazotumiwa katika
      mechi za timu ya taifa, Taifa Stars, kutoka zile
      zilizozoeleka na mashabiki na Watanzania
      wote hadi jezi mpya zinazolalamikiwa na
      mashabiki wengi kuwa hazina mvuto na
      hazionyeshi rangi halisi ya bendera ya taifa la
      Tanzania.

      Jezi mpya ya timu ya taifa ya Tanzania,
      ambayo nayo inatakiwa kubadilishwa
      TFF ilipoamua kutumia jezi mpya
      zinazotumika sasa haikuwashirikisha
      wabunifu wa mavazi kuhusu jezi mpya ya timu
      ya taifa na badala yake ikaja na jezi ambayo
      imekuwa ikilalamikiwa na mashabiki kuwa
      haina mvuto na haiwakilishi rangi halisi za
      bendera ya taifa, huenda ndio maana safari
      hii wametoa tangazo hilo.

      Mbunifu atakayeshinda atapata zawadi ya
      shilingi milioni moja za Kitanzania sawa na
      karibu dola mia saba za Kimarekani kwa
      atakayebuni jezi ya kuchezea mechi za
      nyumbani na vile vile mshindi atakayebuni jezi
      za kuchezea mechi za ugenini naye atapata
      kiasi kama hicho cha fedha.
      Jezi ya sasa ina rangi ya samawati na bluu
      nyeusi.

      • Blogger Comments
      • Facebook Comments

      0 comments:

      Post a Comment

      Item Reviewed: TFF YATAKA JEZI MPYA STARS Rating: 5 Reviewed By: Unknown