728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, November 01, 2014

    TFF YATAKA JEZI MPYA STARS

    Shirikisho la soka Tanzania, TFF, limesema
    linakaribisha wabunifu watakaobuni
    mwonekano wa jezi mpya za timu ya taifa kwa
    mechi za nyumbani na ugenini.
    Hata hivyo sharti la ubunifu huo lazima
    uzingatie rangi za bendera ya taifa ambazo ni
    kijani, njano, nyeusi na bluu.

    Wakati tangazo hili likitolewa na TFF, tayari
    uongozi mpya chini ya rais wake Jamal
    Malinzi umebadili jezi zinazotumiwa katika
    mechi za timu ya taifa, Taifa Stars, kutoka zile
    zilizozoeleka na mashabiki na Watanzania
    wote hadi jezi mpya zinazolalamikiwa na
    mashabiki wengi kuwa hazina mvuto na
    hazionyeshi rangi halisi ya bendera ya taifa la
    Tanzania.

    Jezi mpya ya timu ya taifa ya Tanzania,
    ambayo nayo inatakiwa kubadilishwa
    TFF ilipoamua kutumia jezi mpya
    zinazotumika sasa haikuwashirikisha
    wabunifu wa mavazi kuhusu jezi mpya ya timu
    ya taifa na badala yake ikaja na jezi ambayo
    imekuwa ikilalamikiwa na mashabiki kuwa
    haina mvuto na haiwakilishi rangi halisi za
    bendera ya taifa, huenda ndio maana safari
    hii wametoa tangazo hilo.

    Mbunifu atakayeshinda atapata zawadi ya
    shilingi milioni moja za Kitanzania sawa na
    karibu dola mia saba za Kimarekani kwa
    atakayebuni jezi ya kuchezea mechi za
    nyumbani na vile vile mshindi atakayebuni jezi
    za kuchezea mechi za ugenini naye atapata
    kiasi kama hicho cha fedha.
    Jezi ya sasa ina rangi ya samawati na bluu
    nyeusi.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TFF YATAKA JEZI MPYA STARS Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top