728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, November 08, 2014

    COSTA AIUA LIVEPOOL ANFIELD

    Klabu ya Chelsea imeendeleza wimbi la ushindi baada ya kuifungwa Liverpool kwa magoli 2-1 katika mchezo ulioisha hivi punde katika dimba la Anfield.

    Liverpool ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata goli la kuongoza dakika ya 9 tu ya mchezo baada ya kiungo wake Emre Can kupiga shuti kali lililombabatiza mlinzi wa Chelsea Garry Cahill na kutika wavuni.

    Baada ya goli hilo Chelsea waliamka na kufanikiwa kusawazisha goli hilo kupitia kwa mlinzi Garry Cahill dakika ya 14 na kufanikiwa kupata goli la ushindi dakika ya  67 kupitia kwa mshambuliaji Diego Costa baada ya kazi nzuri toka mlinzi wa kushoto Cesar Azpilicueta.

    Baada ya kichapo hicho Liverpool inajikita nafasi ya nane huku Chelsea ikiwa kileleni kwa pointi 29 pointi 7 dhidi ya klabu ya Southampton iliyoko nafasi ya pili.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: COSTA AIUA LIVEPOOL ANFIELD Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top