728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, November 10, 2014

    MAXIMO KUONGEZA WAWILI YANGA

    BOSI wa Ufundi wa Yanga, Marcio
    Maximo, amesema anataka wachezaji
    wapya wawili tu anaosema wakitua
    klabuni hapo tu basi kazi imeisha na
    ubingwa ataupata kiulaini kabisa, mmoja
    atakuwa mzawa.

    Maximo alisema baada ya kukifanyia
    tathimini kikosi chake amegundua
    kwamba amepungukiwa viungo wawili
    wa kati ambao lazima anunue wapya
    kwenye dirisha dogo la usajili linaloanza
    wikiendi ijayo.

    Alisema katika mapendekezo yake
    anataka Kamati ya Usajili ya timu hiyo
    iliyochini ya Mhandisi Isaac Chanji, Seif
    Ahmed ‘Seif Magari’, Abdallah Bin Kleb
    na Mussa Katabaro, kusaka kiungo mmoja
    mzawa na mwingine wa kigeni huku
    akigoma kutaja majina yao ingawa
    Mwanaspoti lina taarifa za awali.
    “Ukiangalia timu utaona kwamba hakuna
    uwiano sawa kati ya viungo na
    washambuliaji, sasa tuna washambuliaji
    wengi kuliko viungo hiyo sio sawa sana,
    tunahitaji kuongeza watu wawili
    watakaotuongezea nguvu,” alisema
    Maximo ambaye ameondoka nchini leo
    sambamba na wachezaji Wabrazili
    kwenda likizo ya siku 10.

    “Nataka wachezaji wawili tu kwa sasa,
    tayari nimeshawapa majina ya watu
    ninaowataka, siwezi kukutajia ni nani na
    nani, lakini tambua kwamba tayari
    nimeshawasiliana nafikiri mpaka nikirudi
    baada ya siku 10 naweza kuwakuta
    hapa,”alisema Maximo.
    Wakati Maximo akigoma kuwataja,
    Mwanaspoti linafahamu kwamba endapo
    Yanga itamkosa kiungo Jonas Mkude wa
    Simba itahamishia rada kwa Shaban Nditi
    wa Mtibwa Sugar.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MAXIMO KUONGEZA WAWILI YANGA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top