728x90 AdSpace

  • Latest News

      Monday, November 10, 2014

      MAXIMO KUONGEZA WAWILI YANGA

      BOSI wa Ufundi wa Yanga, Marcio
      Maximo, amesema anataka wachezaji
      wapya wawili tu anaosema wakitua
      klabuni hapo tu basi kazi imeisha na
      ubingwa ataupata kiulaini kabisa, mmoja
      atakuwa mzawa.

      Maximo alisema baada ya kukifanyia
      tathimini kikosi chake amegundua
      kwamba amepungukiwa viungo wawili
      wa kati ambao lazima anunue wapya
      kwenye dirisha dogo la usajili linaloanza
      wikiendi ijayo.

      Alisema katika mapendekezo yake
      anataka Kamati ya Usajili ya timu hiyo
      iliyochini ya Mhandisi Isaac Chanji, Seif
      Ahmed ‘Seif Magari’, Abdallah Bin Kleb
      na Mussa Katabaro, kusaka kiungo mmoja
      mzawa na mwingine wa kigeni huku
      akigoma kutaja majina yao ingawa
      Mwanaspoti lina taarifa za awali.
      “Ukiangalia timu utaona kwamba hakuna
      uwiano sawa kati ya viungo na
      washambuliaji, sasa tuna washambuliaji
      wengi kuliko viungo hiyo sio sawa sana,
      tunahitaji kuongeza watu wawili
      watakaotuongezea nguvu,” alisema
      Maximo ambaye ameondoka nchini leo
      sambamba na wachezaji Wabrazili
      kwenda likizo ya siku 10.

      “Nataka wachezaji wawili tu kwa sasa,
      tayari nimeshawapa majina ya watu
      ninaowataka, siwezi kukutajia ni nani na
      nani, lakini tambua kwamba tayari
      nimeshawasiliana nafikiri mpaka nikirudi
      baada ya siku 10 naweza kuwakuta
      hapa,”alisema Maximo.
      Wakati Maximo akigoma kuwataja,
      Mwanaspoti linafahamu kwamba endapo
      Yanga itamkosa kiungo Jonas Mkude wa
      Simba itahamishia rada kwa Shaban Nditi
      wa Mtibwa Sugar.

      • Blogger Comments
      • Facebook Comments

      0 comments:

      Post a Comment

      Item Reviewed: MAXIMO KUONGEZA WAWILI YANGA Rating: 5 Reviewed By: Unknown