728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, November 10, 2014

    MSUVA:KUANZIA BENCHI RAHA SANA

    WINGA mwenye kasi zaidi kwenye kikosi
    cha Yanga, Simon Msuva, amesema
    chachu ya kuifunga Mgambo JKT mabao
    mawili juzi Jumamosi ni yeye kuanzia
    benchi kwani alipata muda mzuri wa
    kuwasoma wapinzani na kufahamu
    mapungufu yao.
    Msuva aliingia kipindi cha pili kwenye
    mchezo huo akichukua nafasi ya Haruna
    Niyonzima na kufanikiwa kufunga mabao
    hayo na kuiwezesha Yanga kuchomoza na
    ushindi wa mabao 2-0 mbele ya kikosi
    cha wachezaji 10 wa Mgambo.
    Winga huyo alisema licha ya kwamba
    Yanga walifanikiwa kushinda, bado
    wapinzani wao walionekana kuwa wazuri
    na kuwapa changamoto kubwa.
    “Nilipokuwa benchi nilifanikiwa
    kuwasoma wapinzani, nilifahamu uzuri
    wao na ubovu wao, hivyo nilivyoingia
    kazi yangu haikuwa ngumu sana,”
    alisema.
    “Kocha pia alinipa maelekezo ya namna
    ya kwenda kupenya kwenye ukuta wa
    wapinzani wetu ambao walionekana
    kuwa imara sana, haikuwa kazi rahisi
    lakini nilijitahidi kupambana.”

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MSUVA:KUANZIA BENCHI RAHA SANA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top