728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, November 04, 2014

    NGASSA AWA MFUNGAJI BORA LIGI YA MABINGWA AFRICA

    MSHAMBULIAJI wa Yanga, Mrisho Ngassa
    amepata zali Afrika, baada ya kumaliza
    kinara wa mabao kwenye Ligi ya
    Mabingwa Afrika, licha ya klabu yake
    kuaga mashindano hayo alfajiri kabisa.
    Ngassa amemaliza kinara baada ya
    kufunga mabao sita na kufungana na
    Ndombe Mubele wa AS Vita Club ya
    Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo,
    Haythem Jouini wa Esperance de Tunis ya
    Tunisia na El Hedi Belameiri wa ES Setif
    ya Algeria.

    Ni baada ya Ligi ya Mabingwa Afrika
    kufikia tamati wikiendi iliyopita na ES
    Setif kutangazwa mabingwa wapya
    wakibebwa na bao la ugenini kutokana na
    matokeo ya sare bao 1-1 mchezo wa
    Algeria na sare mabao 2-2 mchezo
    uliochezwa Kinshasa.

    Ngassa aliyafunga mabao hayo katika
    raundi ya kwanza walipocheza na
    Komorozine ya Comoro mchezo wa
    kwanza walishinda 7-0 na marudiano
    walitoka kifua mbele kwa mabao 5-2.

    Yanga ilitolewa kwenye mashindano na
    Al Ahly ya Misri kwa penalti 3-4. Lakini
    Ngassa hawezi kupewa zawadi yoyote
    kwavile wamefungana na kiutaratibu
    hata mchezaji akishinda tuzo hiyo CAF
    huitoa kwa klabu yake.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: NGASSA AWA MFUNGAJI BORA LIGI YA MABINGWA AFRICA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top