728x90 AdSpace

  • Latest News

      Tuesday, November 04, 2014

      NGASSA AWA MFUNGAJI BORA LIGI YA MABINGWA AFRICA

      MSHAMBULIAJI wa Yanga, Mrisho Ngassa
      amepata zali Afrika, baada ya kumaliza
      kinara wa mabao kwenye Ligi ya
      Mabingwa Afrika, licha ya klabu yake
      kuaga mashindano hayo alfajiri kabisa.
      Ngassa amemaliza kinara baada ya
      kufunga mabao sita na kufungana na
      Ndombe Mubele wa AS Vita Club ya
      Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo,
      Haythem Jouini wa Esperance de Tunis ya
      Tunisia na El Hedi Belameiri wa ES Setif
      ya Algeria.

      Ni baada ya Ligi ya Mabingwa Afrika
      kufikia tamati wikiendi iliyopita na ES
      Setif kutangazwa mabingwa wapya
      wakibebwa na bao la ugenini kutokana na
      matokeo ya sare bao 1-1 mchezo wa
      Algeria na sare mabao 2-2 mchezo
      uliochezwa Kinshasa.

      Ngassa aliyafunga mabao hayo katika
      raundi ya kwanza walipocheza na
      Komorozine ya Comoro mchezo wa
      kwanza walishinda 7-0 na marudiano
      walitoka kifua mbele kwa mabao 5-2.

      Yanga ilitolewa kwenye mashindano na
      Al Ahly ya Misri kwa penalti 3-4. Lakini
      Ngassa hawezi kupewa zawadi yoyote
      kwavile wamefungana na kiutaratibu
      hata mchezaji akishinda tuzo hiyo CAF
      huitoa kwa klabu yake.

      • Blogger Comments
      • Facebook Comments

      0 comments:

      Post a Comment

      Item Reviewed: NGASSA AWA MFUNGAJI BORA LIGI YA MABINGWA AFRICA Rating: 5 Reviewed By: Unknown