728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, November 21, 2014

    SUAREZ KUPOTEZA MANOTI AKING'ATA

    Louis Suarez itabidi awe mpole tu.
    Imegundulika kuwa kama akifanya tena
    ujinga wake wa kung’ata mtu pale Nou
    Camp basi atalambwa dau kubwa la
    mshahara wake wa mwaka, hii ni kwa
    mujibu wa mkataba wake na Barcelona.

    Suarez ambaye ameanza taratibu maisha
    yake ya soka Barcelona anachukua dau la
    pauni 10 milioni kwa mwaka, lakini
    inadaiwa kuwa atakatwa dau la pauni 3
    milioni kama akimng’ata mchezaji wa
    timu pinzani.

    Nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay
    tayari amewang’ata wachezaji watatu
    katika maisha yake ya soka akichezea
    klabu za Ajax, Liverpool na timu yake ya
    taifa ya Uruguay.
    Novemba 20, 2010 alimng’ata mchezaji
    wa PSV, Otman Bakkal katika pambano la
    Ligi Kuu ya Uholanzi lililomalizika kwa
    suluhu ya bila kufungana. Klabu yake ya
    Ajax ilimsimamisha mechi mbili na
    kumtoza faini.

    Kama vile haitoshi, April mwaka jana
    alimng’ata mlinzi wa Chelsea, Branislav
    Ivanovic katika pambano la Ligi Kuu ya
    England uwanja wa Anfield. FA
    ilimfungia mechi 10 za Ligi Kuu ya
    englad.
    June mwaka huu alimalizia Hat trick
    yake ya kung’ata wakati alipomng’ata
    mlinzi wa timu ya taifa ya Italia, Giorgio
    Chielini katika pambano la kombe la
    dunia nchini Brazil. Alifungiwa kucheza
    soka kwa miezi minne huku akifungiwa
    mechi kumi za timu yake ya taifa ya
    Uruguay.

    Hata hivyo, baada ya uhamisho huo, staa
    huyo alikamilisha uhamisho wa pauni 75
    milioni kwenda Nou Camp kutoka Anfield
    huku akiingia mkataba wa miaka mitano
    ambayo unamfanya alipwe mshahara wa
    pauni 200,000 kwa wiki.

    Mshahara huo
    unamfanya awe mchezaji wa nne kwa
    kulipwa zaidi katika klabu ya Barcelona
    nyuma ya Lionel Messi, Neymar na
    Andres Iniesta, lakini huenda ukashuka
    maradufu kama akiendeleza tabia zake za
    Ajax na Liverpool.

    Mkataba wa Barcelona kwa Suarez ni
    mkali na utamuona mchezaji huyo
    akipoteza kiasi cha asilimia 15 hadi 30 ya
    mshahara kama akirudia kung’ata
    wachezaji wa timu pinzani.
    Hata hivyo, inadaiwa kuwa mabosi wa
    Barcelona kwa kiasi kikubwa
    walishukuru kitendo cha Suarez
    kumng’ata Chiellini kwa sababu kwa
    kiasi kikubwa kiliharakisha mazungumzo
    kati ya timu yao na Anfield.
    Kitendo hicho kilishusha thamani ya
    Suarez kwa kiasi kikubwa na ni timu
    chache ambazo ziliamua kufukuzia saini
    yake mara baada ya kung;ata nchini
    Brazil.

    Kuhakikisha kwamba tukio hilo halitokei
    tena, hivi karibuni nyota huyo amekiri
    kwamba kwa sasa anapata msaada wa
    matibabu ya kisaikolojia kuhakikisha
    kwamba hawezi kufanya tena kitendo
    hicho katika siku za karibuni.
    “Baada ya kufungiwa nilikuwa na wakati
    mgumu sana. Napata msaada wa
    kisaikolojia na klabu imekuwa ikinisapoti
    sana.” alisema mchezaji huyo mwenye
    mke na watoto wawili.

    Hata hivyo, Suarez amekuwa akipata
    sapoti kutoka kwa wanamichezo
    mbalimbali duniani licha ya tabia yake
    hiyo ya kung’ata. Mmoja kati ya
    wanamichezo ambao wamemuunga
    mkono ni bondia wa zamani wa uzito wa
    Juu Mike Tyson.
    “Nadhani zilikuwa hasira za muda tu,
    kichwa kilipata moto baada ya
    mapambano. Ni suala la kushindwa
    kumiliki hasira za muda tu.

    Tunakuwa na
    hasira za kiushindani na tunakosea
    kufikiria vizuri. Wakati mwingine
    unachanganyikiwa.” Alisema Tyson.
    Tyson mwenyewe aliwahi kukumbwa na
    kashfa ya kumng’ata bondia mwenzake
    wa uzito wa juu wa Marekani, Evander
    Holyfiekld mnamo June 28, 1997.
    Mwingine aliyemtetea Suarez alikuwa
    mkongwe wa soka duniani, Diego
    Maradona ambaye alishutumu zaidi
    kifungo cha miezi minne ambacho Suarez
    alipewa na Fifa mara baada ya kumng’ata
    Chiellini.

    “Uamuzi huo ni fedhea. Siwezi kuelewa
    kwanini. Suarez amemuua nani hadi
    apewe kifungo hiki? Kwanini Fifa
    wasimtie pingu na kumpeleka
    Guantanamo Bay?” alihoji Maradona
    ambaye anasifika kwa misimamo yake ya
    kuipinga Fifa mara kwa mara.
    “Mchezaji anafanya kazi ngumu mwaka
    mzima hili acheze kombe la dunia, Luis
    alifunga mabao 29 na wamemuondoa
    kombe la dunia kama hivi. Inashangaza
    sana.”

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SUAREZ KUPOTEZA MANOTI AKING'ATA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top