728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, November 04, 2014

    NANI:SIRUDI MANCHESTER UNITED NG'O

    WINGA Nani hafikirii kabisa kurudi
    Manchester United. Mchezaji huyo
    alikwenda Sporting Lisbon kwa mkopo na
    kamwe haoni dalili ya kurudi kwenye
    kikosi chake.

    Ni wazi kuwa kocha mpya wa Man United
    Louis van Gaal wala hamfuatilii sana na
    Nani ameibuka na kusema hana mpango
    na klabu hiyo.

    Gazeti moja la Ureno la O Jogo lilimkariri
    akitamka: “Ukweli ni kwamba wala sina
    mpango wa kurudi kwenye kikosi cha
    Man United. Nawapenda watu
    wanaonipenda, naamini watu
    wanaoamini kuwa nina uwezo wa
    kufanya vizuri.

    “Nikiwa hapa (Sporting Lisbon) kila
    ninapoamka najiona mwenye nguvu zaidi,
    kuna viongozi wanaofahamu kuwa nina
    uwezo mkubwa na wanataka nionyeshe
    kiwango zaidi,” alisema mchezaji huyo
    mwenye miaka 27.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: NANI:SIRUDI MANCHESTER UNITED NG'O Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top