728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, November 17, 2014

    PIGO UNITED,BLIND NJE YA DIMBA WIKI SITA

    Klabu ya Manchester United imepata pigo jingine baada kiungo wake Muholanzi Delay Blind 24 kupata majeraha jana jumapili wakati akiitumikia timu yake ya taifa dhidi ya Latvia katika mchezo wa kusaka tiketi ya kucheza michuano ijayo ya Ulaya `Euro 2016'

    Blind aliumia misuli kipindi cha kwanza kufuatia kuchezewa vibaya na kiungo wa Latvia Eduards Visnakovs na nafasi yake kuchukuliwa na kiungo wa  Feyenoord Jordy Clasie katika mchezo ulioisha kwa Uholanzi kuitandika Latvia kwa jumla ya mabao 6.

    Habari kutoka chama cha soka cha nchi hiyo zinadai kuwa kiungo huyo anayetumia guu la kushoto dimbani atakuwa nje kwa kipindi cha wiki nne mpaka sita hivyo kuikosa safari ya Emirates kuivaa Arsenal.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: PIGO UNITED,BLIND NJE YA DIMBA WIKI SITA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top