728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, November 13, 2014

    RONALDO:SIJAWAHI KUMTUSI MESSI

    JOTO la upinzani kati ya staa wa Real
    Madrid, Cristiano Ronaldo na nyota wa
    Barcelona, Lionel Messi sasa linaingia
    katika uhasama baada ya kudaiwa kuwa
    Ronaldo amekuwa akimtukana Messi
    pindi akiwa na wachezaji wenzake wa
    Real Madrid.

    Mwandishi mahiri wa michezo wa
    Hispania, Guillem Balague ameandika
    katika kitabu chake kuwa Ronaldo
    amekuwa akimtukana Messi kwa majina
    tofauti na habari hiyo imezua zogo kubwa
    nchini Hispania.

    Hata hivyo, Ronaldo amesisitiza kupitia
    mtandao wake kwamba habari hizo siyo
    za kweli na hajawahi kumtukana Messi,
    huku akitishia kuchukua hatua za
    kisheria.

    “Habari zinazunguka zikinishutumu
    kwamba nimekuwa nikitoa maneno
    machafu dhidi ya Lionel Messi. Habari
    hizi ni za uongo na nimemwambia
    mwanasheria wangu achukue hatua kwa
    wote wanaohusika,” aliandika Ronaldo
    katika mtandao wake.

    “Nina heshima kubwa kwa wanasoka
    wenzangu wote wa kulipwa na Messi
    hana tofauti na nao,” aliongeza Ronaldo
    mwenye umri wa miaka 29 kwa sasa.

    Katika kitabu cha Balague, ameelezea
    uhusiano baina ya wachezaji hao wawili
    akidai kwamba hawana urafiki wowote
    lakini wamekuwa wapole mbele ya jamii
    kwa ajili ya kuvifurahisha vyombo vya
    habari.

    Mwandishi huyo mkongwe amedai
    kwamba wachezaji kadhaa wa Real
    Madrid wamempa taarifa kwamba siyo tu
    Ronaldo amekuwa akimtukana Messi peke
    yake, bali mtu yeyote anayemuona
    anaongea na Messi.

    “‘Ronaldo, labda kwa kuonyesha dalili za
    kutopevuka kama ilivyo kwa wanasoka
    wengi wa sasa, anadhani kuna umuhimu
    wa kuweka sura ya kishujaa mbele ya
    wachezaji wenzake na kutomhofia Messi
    kwa ajili ya kupambana naye,” anaandika
    Balague.

    “Lakini yote hayo ni uongo na ndio
    maana, kwa mujibu wa baadhi ya
    wachezaji wa Real Madrid, Ronaldo
    amekuwa akimtukana Messi kwa matusi
    mbalimbali na akimuona mtu yeyote
    klabuni kwao anaongea na Messi huwa
    anaishia kumtukana.”
    Kwa sasa Ronaldo yupo katika kikosi cha
    Ureno akijiandaa na mechi za kufuzu kwa
    Euro 2016 ambapo kesho wanakipiga
    dhidi ya Armenia.

    Messi jana alikuwa anatarajiwa kuiongoza
    Argentina dhidi ya Croatia katika Uwanja
    wa West Ham, Rush Green.
    Wawili hao wanatazamiwa kukumbana
    uso kwa uso Jumanne ya wiki ijayo katika
    pambano la kirafiki baina ya nchi zao
    litakalopigwa katika Dimba la Old
    Trafford.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: RONALDO:SIJAWAHI KUMTUSI MESSI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top