728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, November 07, 2014

    OKWI:SINA TATIZO NA TAMBWE

    STRAIKA aliyechukua hatamu kwenye
    fowadi ya Simba, Mganda Emmanuel
    Okwi, amesisitiza kwamba hana tofauti na
    mchezaji yeyote wa Simba na anatamani
    kucheza pamoja na mshambuliaji
    anayeanzia benchi, Mrundi Amissi
    Tambwe.

    Thamani ya Tambwe ambaye alikuwa
    straika namba moja wa Simba msimu
    uliopita, imeshuka kutokana na mfumo
    wa kocha Mzambia Patrick Phiri ambao
    umemfanya aanzie benchi ingawa katika
    mchezo wa Jumapili dhidi ya Ruvu
    Shooting kwenye Uwanja wa Taifa ana
    nafasi kubwa ya kuanza.
    Tambwe ambaye alikuwa mfungaji bora
    msimu uliopita, sasa anaanzia benchi na
    Phiri anapenda kumtumia zaidi Okwi kwa
    maelezo kwamba ana kasi, nguvu na
    anajua kutumbukiza mipira nyavuni
    tofauti na staili ya Tambwe ambaye ni
    mviziaji na akikutana na mabeki wabishi
    timu hukwama.

    Ingawa uongozi umekanusha kwa nguvu,
    lakini kumekuwa na maneno kwamba
    thamani ya Tambwe ndani ya Simba
    imeshuka baada ya Okwi kutua na
    kwamba mchezaji huyo anafikiria kuingia
    mitini kwenye dirisha dogo la usajili
    litakaloanza Novemba 15 licha ya
    kwamba uongozi unajitahidi kumuweka
    fiti kisaikolojia.

    Okwi aliyetua Simba akitokea Yanga
    aliyositisha nayo mkataba, alisema hana
    tatizo katika kucheza na Tambwe katika
    kikosi cha kwanza na Phiri amekiri
    kwamba atawapanga.
    Okwi alisema anapocheza na Tambwe
    katika kikosi kimoja safu ya ushambuliaji
    yao inakuwa na makali zaidi. “Sina tatizo
    katika kucheza na Tambwe pale mbele
    wala mchezaji mwingine yeyote,
    nakumbuka kuna mechi tuliyocheza
    pamoja mimi na Tambwe tulielewana
    sana nikajikuta nimebanwa na mabeki
    lakini Tambwe akawa sehemu safi
    nikampa krosi akafunga kirahisi
    kabisa,”alisema Okwi ambaye amekuwa
    akijituma sana katika mechi za
    hivikaribuni mpaka kufikia hatua ya
    kucheza na majeraha.

    Kwa upande wake Phiri alisema: “Kuna
    mechi nakumbuka walicheza pamoja
    Tambwe akafunga, lakini hapa kati
    sikuwa nawapanga pamoja kuna mambo
    nilikwa najaribu kuyapanga sasa Okwi
    anaumwa lakini akipona tutaangalia
    uwezekano wa kuweza kuwatumia tena
    kucheza pamoja katika mechi ijayo.”
    Katika mazoezi ya juzi Jumatano ya kikosi
    hicho, Phiri alionekana kumjaribu
    Tambwe katika kikosi ambacho kinaweza
    kuanza Jumapili huku Okwi akianza
    mazoezi taratibu peke yake ambapo
    uwezekano wa kuwepo mechi ijayo
    itategemea na maendeleo ya maumivu
    yake.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: OKWI:SINA TATIZO NA TAMBWE Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top