728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, June 30, 2017

    WAGOMBEA 29 WAFANYIWA USAILI SIKU YA KWANZA TFF


    Dar Es Salaam.

    Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limefanya usaili kwa wagombea 29 wa nafasi mbalimbali katika siku ya kwanza ya hatua hiyo muhimu kuelekea uchaguzi mkuu wa shirikisho.

    Kabla ya usaili, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Revocatus Kuuli, aliwatangazia wagombea wote kuwa amepokea mapingamzi mawili ambayo ni:-

    Hussein Mwamba ambaye ni Mjumbe kwa sasa wa Kamati ya Utendaji ya TFF, aliyempinga Mussa Sima kuwa amejitokeza kuwania nafasi hiyo katika Kanda ya 10 ya Mikoa ya Dodoma na Singida kuwa hana uzoefu wa miaka mitano.

    Wanafamilia wote kwa maana ya Mwamba na Sima walikuwako. Wakaitwa kikaoni, lakini mweka pingamizi - Mwamba aliamua kulitoa pingamizi lake.

    Pingamizi jingine ambalo liliwekwa leo ni kwa Mgombea nafasi ya urais John Kijumbe ambaye anapinga Wallace Karia - Makamu Rais kwa sasa wa TFF kwamba hana sifa za kuwania urais wa TFF kama alivyoomba.

    Hata hivyo, pingamizi hilo halijasikilizwa kwa sababu ya wahusika wote kutokuwako na baada ya kamati kufanya nao mawasiliano, wametangaza kusikiliza pingamizi hilo Jumamosi ambayo ni siku ya mwisho ya usaili.

    Wagombea ambao wamesailiwa leo hadi jioni ya leo Alhamisi kwa upande wa wagombea urais ni Imani Madega na Ally Mayay wakati Wagombea Makamu urais waliosailiwa ni Mtemi Ramadhani na Mulamu Nghambi.

    Kanda Na. 1 Mikoa ya Kagera na Geita;

    Soloum Chama

    Kaliro Samson

    Leopold Mukebezi

    Kanda Na. 2 Mikoa ya Mara na Mwanza;

    Aaron Nyanda 

    Samwel Daniel

    Bado

    Vedastus Lufano

    Ephraim Majinge

    Kanda Na. 3 Mikoa ya Shinyanga na Simiyu;

    Mbasha Matutu

    Bado

    Benista Rugora

    Stanslaus Nyongo

    Kanda Na. 4 Mikoa ya Arusha na Manyara; 

    Wote Bado

    Omari Walii

    Sarah Chao

    Peter Temu

    Kanda Na. 5 Mikoa ya Kigoma na Tabora;

    John Kadutu

    Bado

    Issa Bukuku

    Abubakar Zebo

    Francis Michael

    Kanda Na. 6 Mikoa ya Katavi na Rukwa;

    Baraka Mazengo

    Bado

    Kenneth Pesambili

    Kanda Na. 7 Mikoa ya Mbeya, Songwe na Iringa;

    Elias Mwanjala

    Cyprian Kuyava

    Bado

    Erick Ambakisye

    Abousuphyan Silliah

    Kanda Na. 8 Mikoa ya Njombe na Ruvuma;

    Wote bado

    James Mhagama

    Golden Sanga

    Vicent Majili

    Yono Kevela

    Kanda Na. 9 Lindi na Mtwara;

    Wote Bado

    Athuman Kambi

    Dunstan Mkundi

    Kanda Na. 10 Mikoa ya Dodoma na Singida; 

    Hussein Mwamba

    Mohamed Aden

    Musa Sima

    George Benedict Komba

    Bado

    Stewart Masima 

     Ally Suru

    Kanda Na. 11 Mikoa ya Pwani na Morogoro;

    Gabriel Mkwawe

    Bado

    Charles Mwakambaya

    Francis Ndulane

    Hassan Othman ‘Hassanol’ 

    Kanda ya 12. Mikoa ya Kilimanjaro na Tanga

    Khalid Mohamed

    Bado

    Goodluck Moshi

    Thabit Kandoro

    Kanda Na. 13 Mkoa wa Dar es Salaam

    Emmanuel Ashery

    Shaffih Dauda

    Mussa Kisoky

    Lameck Nyambaya

    Jamhuri Kihwelo

    Saad Kawemba

    Bado

    Bakari Malima

    Ayoub Nyenzi

    Saleh Alawi

    Ramadhani Nassib

     Aziz Khalfan

    Abdul Sauko

    Peter Mhinzi

    Ally Kamtande

    Said Tully

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WAGOMBEA 29 WAFANYIWA USAILI SIKU YA KWANZA TFF Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top