728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, June 22, 2017

    KALENDA:Kozi ya waamuzi yasogezwa mbele

    Dar Es Salaam,Tanzania.

    Kozi ya waamuzi wa mpira wa miguu, iliyolenga kuwainua madaraja kutoka madaraja waliyonayo sasa hadi ngazi moja juu, imesogezwa mbele kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi ya TFF, Saloum Chama.
    Chama amesema kwamba kozi hiyo iliyopangwa kufanyika kuanzia Juni 29, mwaka huu itafanyika hapo baadaye katika tarehe itakayopangwa, lakini itakuwa ni kabla ya Uchaguzi Mkuu wa TFF.
    “Watu wasiende kuripoti hiyo Juni 29, mwaka huu kama tulivyotangaza. Tumesogeza mbele kidogo kozi hii. Tarehe mpya itatangazwa hapo baadaye,” amesema Chama ambaye alitaja vituo vilivyopangwa kuwa ni Mwanza, Ruvuma na Dodoma.

    TANGAZA BIASHARA YAKO NASI Simu : + 255 675 734 252 + 255 717 705 548 Email : sokaextra82@gmail.com
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KALENDA:Kozi ya waamuzi yasogezwa mbele Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top