728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, April 16, 2016

    WAYNE ROONEY AWAPONZA WALCOTT,CHAMBERLAIN ENGLAND

    London,England.

    AMETIBUA!!Kurejea uwanjani kwa nyota wa Manchester United Wayne Rooney kumemfanya kocha Roy Hodgson kuwaengua nyota wa Arsenal Theo Walcott na Alex Oxlade-Chamberlain katika kikosi cha England kitakachokwenda kushiriki katika kinyang'anyiro cha kombe la mataifa ya Ulaya (Euro 2016) huko Ufaransa mwezi Juni mwaka huu.

    Kwa mujibu wa gazeti la The Daily Mirror  ni kuwa Hodgson ameamua kuwa atamtumia Wayne Rooney,31 katika nafasi ya winga ya kulia badala ya ushambuliaji kama ilivyozoeleka.

    Katika nafasi ya ushambuliaji Hodgson atawatumia nyota wawili wa Tottenham Harry Kane na Dele Alli huku Danny Welbeck akitumika kama winga wa kushoto.

    Winga ya kulia ambayo ndiyo kimbilio la Walcott na Alex Oxlade-Chamberlain huku kutakuwa na nahodha Wayne Rooney,Jamie Vardy na Raheem Sterling.

    Hivyo basi hii ina maana kuwa Theo Walcott na Alex Oxlade-Chamberlain hawatakuwa na chao/nafasi katika mshindano ya mwaka huu ya mataifa ya Ulaya.

    Taarifa za ndani zinasema Roy Hodgson amelazika kumchukua Wayne Rooney kutokana na kuwa na uzoefu mkubwa katika michuano ya kimataifa.Ikumbukwe pia nyota huyo wa Manchester United ndiye anayeshikilia rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote wa England baada ya kuvunja rekodi ya Sir Bobby Charlton.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WAYNE ROONEY AWAPONZA WALCOTT,CHAMBERLAIN ENGLAND Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top