728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, April 26, 2016

    HIZI HAPA HABARI KUBWA 12 ZA USAJILI TOKA ULAYA JIONI YA JUMANNE YA LEO

    Taison-Wellington

    Kane:Diego Maradona ameishauri klabu yake ya zamani ya Napoli kumsajili mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane,22 ikiwa itaamua kumuuza mshambuliaji wake wa sasa Muargentina Gonzalo Higuain,30.(Piuenne)

    Depay:West Ham imeungana na vilabu vya Paris Saint-Germain, Monaco na Liverpool katika mbio za kuisaka saini ya winga wa Manchester United Mdachi Memphis Depay22.(transfermarketweb).com

    Falcao:Roma imefungua mazungumzo na Monaco kwa ajili ya kutaka kumsajili mshambuliaji Mcolombia Radamel Falcao,31.Ripoti toka Italia zinadai ili kufanikisha dili hilo Falcao atatakiwa kupunguza mshahara wake wa £100,000 kwa wiki.(Daily Mirror)

    Taison:Arsenal imeripotiwa kuanza kuwatolea macho ya kutaka kuwasajili nyota wawili wa Shaktar
    Donetsk Wabrazil Taison na Wellington.

    Fellaini:AS Roma imeripotiwa kuandaa kitita cha £15m ili kumsajili kiungo wa Manchester United Marouane
    Fellaini,28.(Gazzetta dello Sport)

    Haidara:Chelsea ina matumaini makubwa ya kuipiku Bordeaux katika mbio za kuiwania saini ya kinda toka Mali Amadou Haidara.Haidara,17 ana milikiwa na shule ya kukuza vipaji ya JMG Academy.(L’Equipe) 

    Rodgers: Swansea imeripotiwa kuwa tayari kumpa kocha wake wa zamani Brendan
    Rodgers ofa ya £4m kwa mwaka ili arejee kuifundisha.(The Sun)

    Chamberlain:Kaka mdogo wa winga wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain aitwaye Christian Oxlade-Chamberlain amepewa mkataba wa kwanza wa kulipwa na klabu yake ya Portsmouth.(Daily Star)

    Boyko:Everton imeripotiwa kuandaa £4m kwa ajili ya kumsajili mlinda mlango asiye na nafasi katika klabu ya Besiktas Mukraine Denys Boyko ili kuchukua nafasi ya Tim
    Howard anayetarajiwa kuondoka mwishoni mwa msimu huu.

    Martinez: Mlinzi wa kati wa Real Sociedad Inigo Martinez,24 ameachana na mpango wa kutaka kuhamia Liverpool na badala yake amesaini mkataba mpya wa kuendelea kubakia Anoeta.(AS)

    Mahrez:Mshindi wa tuzo ya PFA Mualgeria Riyad,25 Mahrez ameripotiwa kukataa ofa ya kutua Paris Saint-Germain kwa madai kuwa ana mapenzi makubwa na ligi kuu ya England.

    Vermaelen:Barcelona imeripotiwa kujiandaa kuwatupia virago walinzi wake watano hapo mwishoni mwa msimu huu.Walinzi hao ni Douglas, Adriano,Dani Alves na Thomas Vermaelen pamoja na Marc Bartra.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: HIZI HAPA HABARI KUBWA 12 ZA USAJILI TOKA ULAYA JIONI YA JUMANNE YA LEO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top