728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, April 23, 2016

    MAN UNITED YAONGOZA KUMWAGA PESA KWA MAWAKALA

    Manchester, England.

    Manchester United imetajwa kuwa ni klabu iliyotumia pesa nyingi zaidi kuwalipa mawakala wa wachezaji kuliko vilabu vingine vyote vya ligi kuu nchini England katika kipindi cha kati ya Octoba 1 2015 na Februari 1,2016. 

    Katika ripoti hiyo iliyotolewa siku ya Ijumaa Manchester United imeripotiwa kutumia zaidi ya £10m licha ya kushindwa kufanya usajili wowote katika kipindi hicho huku pia ikishindwa kuwapa mikataba mipya nyota wake mbalimbali.

    Katika kipindi cha Octoba mpaka Februari Manchestet United imefanikiwa kuwauza Ben Pearson na Liam Grimshaw kwenda Preston huku ikitoa kwa mkopo jumla ya nyota wake sita wakiwemo mshambuliaji James Wilson na mlinda mlango Victor Valdes.

    Vilabu vingine vilivyotajwa kumwaga pesa kwa ajili ya kulipa ada za mawakala ni Liverpool, Manchester City na Arsenal.

    Orodha kamili iko kama ifuatavyo:

    1. Manchester United £10,023,318
    2. Liverpool £6,672,713
    3. Manchester City £5,880,098
    4. Arsenal £3,135,483
    5. West Ham United £2,691,331
    6. Tottenham £2,562,853
    7. Chelsea £2,214,227
    8. Stoke City £1,748,093
    9. West Bromwich Albion £1,700,127
    10. Aston Villa £1,638,571
    11. Bournemouth £1,451,647
    12. Crystal Palace £1,197,845
    13. Norwich £1,183,890
    14. Leicester £936,004
    15. Southampton £799,750
    16. Watford £782,494
    17. Sunderland £733,894
    18. Newcastle £538,107
    19. Swansea £491,000
    20. Everton £471,400



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MAN UNITED YAONGOZA KUMWAGA PESA KWA MAWAKALA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top