728x90 AdSpace

Friday, May 29, 2015

UMAPECANO ATUA MAN UTD,GUNDOGAN APEWA ULAJI BAYERN

Kovacic:Klabu ya Liverpool imeripotiwa kuitaka saini ya nyota wa Inter Milan Mateo Kovacic kwa ada ya €18m ili kuimarisha safu yake ya kiungo.

Gundogan:Klabu ya Bayern Munich imeripotiwa kuandaa mshahara wa €8m kwa mwaka na mkataba wa miaka mitatu kwa kiungo wa Borussia Dortmund Illikay Gundogan.

Ancellotti:Kutoka Italia habari zinasema klabu ya Ac Milan inajiandaa kuachana na kocha wake wa sasa Felipe Inzagi na kumuajiri Carlo Ancellotti.Milan imeandaa €86m kwa ajili ya kusuka upya kikosi chake.

Gueye:Klabu ya Southampton imeripotiwa kuwa katika mazungumzo na klabu ya Lille kwa ajili ya kumsajili kiungo Idrissa Gueye kwa ada ya €10m ili kuziba pengo la kiungo wake Morgan Schneiderlin anayetarajiwa kutimka katika kipindi hiki cha usajili barani Ulaya.

Upamecano:Klabu ya Manchester United imeshinda mbio za kumuwania kinda wa kifaransa toka klabu ya Valenciennes Dayot Upamecano (16).Ili kukamilisha dili hilo United italazimika kulipa kitita cha €450,000.

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: UMAPECANO ATUA MAN UTD,GUNDOGAN APEWA ULAJI BAYERN Rating: 5 Reviewed By: Unknown