728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, May 28, 2015

    SEVILLA KIBOKO YATWAA EUROPA,YATINGA LIGI YA MABINGWA

    Sevilla,Hispania.

    Mabao mawili yaliyofungwa na mshambuliaji hatari Carlos Bacca jana usiku yalitosha  kuipa Sevilla  Kombe la Europa ligi mbele ya klabu ya Ukraine FC Dnipro Dnipropetrovsk kwa bao 3-2 katika mchezo wa fainali uliyochezwa katika dimba la  National Stadium huko Warsaw,Poland.

    Sevilla inaweka historia ya kuwa klabu ya kwanza kutwaa taji hilo mara nne.Sevilla ilitwaa taji hilo mara ya kwanza mwaka 2006, 2007,2014 na 2015.

    Kufuatia ushindi huo wa jana usiku Sevilla inajipatia tiketi ya kushiriki ligi ya mabingwa msimu ujao baada ya sheria mpya ya UEFA kuagizwa hivyo kwa bingwa wa ligi ya Europa.

    Kufuatia Sevilla kupata nafasi hiyo nchi ya Hispania itawakilishwa na vilabu vitano katika ligi ya mabingwa ambavyo ni Real Madrid,Barcelona,Atletico Madrid,Valencia na Sevilla.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SEVILLA KIBOKO YATWAA EUROPA,YATINGA LIGI YA MABINGWA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top