728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, September 07, 2015

    FERGUSON:MAZUNGUMZO YA BAFUNI YALIFANYA NIMSAJILI ERIC CANTONA

    Manchester,England.

    Unaweza kudhani kuwa ni utani au mzaha toka kwa kocha wa zamani Manchester United Alex Ferguson juu ya jinsi alivyofikia uamuzi wa kumsajili gwiji wa Kifaransa Eric Cantona.

    Ferguson kutoka katika kitabu chake kiitwacho Leading amefichua kwamba alimsajili Cantona baada ya kusikiliza mazungumzo (uchambuzi) yaliyokuwa yakifanywa na wachezaji wake Steve Bruce na Gary Pallister wakati wakioga baada ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Leeds United mwaka 1992.

                                                                    Cole na Cantona

    Anasema "Niliamua kuungana na wachezaji wangu kuoga pamoja kitu ambacho hakikuwa kawaida yangu kufanya hiyo.Nilikuwa nikifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Bruce na Pallister kuhusu mchezo tuliokuwa tumetoka kuucheza.Wote wawili walikuwa wakisifia mchezo mzuri ulionyeshwa na Cantona ambaye ndiyo kwanza alikuwa amejiunga na Leeds Akitokea Nimes.Alimaliza Ferguson

    Gary Pallister and Eric Cantona of Manchester United celebrate with the FA Cup in the dressing room after the Chelsea v Manchester United FA Cup Final match
                                                   Pallister na Cantona wakiwa na taji la FA

    Cantona aliifungia Manchester United jumla ya mabao 82 katika michezo 185 baada ya kudumu kwa miaka mitano huku akitwaa mataji manne ya ligi kuu pamoja na mataji ya FA.
    Manchester United's Eric Cantona jumps into the crowd with his infamous Kung-Fu kick on a Palace supporter after being sent-off
    Cantona akimchapa kiatu shabiki aliyemtusi
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: FERGUSON:MAZUNGUMZO YA BAFUNI YALIFANYA NIMSAJILI ERIC CANTONA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top